Monday, October 17, 2011

DKT. MKOMBOZI MTAFITI NA MTAALAMU WA
TIBA ASILIA TANZANIA


* Abainisha chanzo na tiba ya kukosa nguvu za Kiume / Uzazi

TATIZO la kukosa nguvu za kiume na maumivu ya juu ya kitovu kwa wanaume na wanawake ni matatizo ambayo yamekuwa yakiwasumbua watu wengi hapa nchini na hata nje ya nchi.

Kutokana na matatizo hayo, zimefanyika tatifi nyingi ili kubaini chanzo chake.

Hata hivyo pamoja na tafiti hizo zipo ambazo zimezaa matunda huku nyingine zikigonga mwamba.

Hali hiyo imewafanya wataalamu mbalimbali wa afya kuumiza vichwa ili kuhakikisha inapatikana tiba mbadala ya kukabiliana na tatizo hilo.

Dkt Cleofas Lucas Kasonso ni kati ya watafiti walioumiza vichwa vyao ili kusaka tiba hiyo na katika makala haya pamoja na mambo mengine anaelezea chanzo cha matatizo hayo.

Anasema, zipo sababu nyingi ambazo kwa kiasi kikubwa zinazosababisha tatizo hilo na kati ya sababu hizo ni kutahiriwa katika umri mdogo au umri mkubwa kwa upande wa wanaume.

“Hili ni moja ya sababu ambayo inaweza kumsababishia mwanaume kukosa nguvu za kiume na kutoweza kushiriki tendo la ndoa, “anasema Dkt. Mkombozi.

Dkt. Mkombozi anasema mbali na sababu hizo, pia maradhi ya zinaa na kujichua huathiri sana sehemu za via za uzazi hivyo kumfanya mwanaume kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa na kutokuwa na uwezo kabisa.

Akifafanua matatizo yanayosababishwa na kutahiriwa katika umri mdogo ambao ni kati ya miezi sita hadi miaka mitatu, Dkt. Mkombozi anasema kuwa watu wa umri huo hujikuta wakipata mshutuko wa viungo vya mwili hususani sehemu za siri na hivyo kusababisha kutokuwa na hisia za kutosha katika kushiriki tendo la ndoa.

“Hali hiyo inaweza kuanza kupoteza hisia pale mtu anapoingia katika balehe ya kwanza, na inaweza kutokea hisia kuja na kupotea wakati wa tendo la ndoa kwani wakati wa tohara mtu uhumia sana sehemu za chini ya uume kwenye mshipa mkubwa sehemu ya kibofu cha mkojo,” anasema Dkt. Mkombozi.

Anasema pia madhara kama hayo huwapata watu wanaotahiriwa katika umri mkubwa kuanzia miaka 16 hadi 50, lakini kwa watu wenye umri kama huu hujikuta wakikumbwa na madhara mengine ambayo ni kuwa na hisia nyingi za kutaka kushiriki tendo la ndoa wakati akiwa bado na kidonda.


Anasema, mbali na matatizo hayo, sehemu zake za uume zitakuwa zinasimama sana na hivyo kumsababishia kupata maumivu ya mishipa.

Dkt. Mkombozi anasema pia baada ya kupona mwathirika wa tatizo hilo atakuwa na hamaki ya kufanya tendo la ndoa lakini nguvu zake zitakuwa zinapungua siku hadi siku.

“Ikitokea ana mwili mkubwa maumbile yake yatanywea na kurudi ndani na kama atakuwa mwembamba wa wastani maumbile yatakuwa membamba mno na yasiyokuwa na nguvu kabisa huku yakiwa yamelegea,” anasema Dkt. Mkombozi.

Kwa upande wa kina mama Dkt. Mkombozi anasema kwa mwanamke aliyewahi kubakwa katika umri mdogo au hata umri mkubwa naye hujikuta hana hisia yoyote ya kutaka kushiriki tendo la ndoa.

Mbali na kubakwa Dkt. Mkombozi anasema kuwa matatizo haya pia huwakumba wanawake waliotolewa bikra na wanaume wenye sehemu za siri zenye maumbile makubwa au wengine ambao hawajawahi kuona bikra zao.

Dkt. Mkombozi anasema, hali hiyo inatokana na mwanamke kupatwa na mshutuko mkubwa kwa kuingiliwa kwa nguvu bila kutayarishwa ama bila hiyari yake.

“Hali hii itamfanya kupata mshutuko wa viungo vya uzazi hasa kizazi chenyewe kuvurugika na kusababisha kutopata hamu ya kushiriki tendo la ndoa kwa muda mrefu sana,” anasema Dk. Mkombozi.

Anasema, kwa upande wa mwanamke ambaye ametolewa bikra na mwanaume mwenye sehemu za siri zenye maumbile makubwa hali hiyo humsababishia kutokuwa na msisimko wa kutosha katika tendo la ndoa na kuvurugika kwa hedhi.

Dkt. Mkombozi anasema, kwa mwanamke ambaye hakuwahi kuona bikra ataweza kupata watoto au asipate, lakini uwezo wake wa kushiriki tendo la ndoa utakuwa ni mdogo sana, au anaweza kushiriki vyema lakini hatosheki na atakuwa anahitaji kufanya tendo hilo kila wakati ama kujamiiana na wanaume wengi kwa pamoja.

Anasema hali hiyo itamfanya kufanana na yule aliyetolewa bikra na mwanaume mwenye sehemu za siri zenye maumbile makubwa sambamba na yule aliyebakwa.

Dkt. Mkombozi anasema, matatizo mengine yanayowakumba watu wa aina hiyo ni kiuno kuuma, mgongo na tumbo kujaa gesi na kuunguruma na miguu kuwa na ganzi na kuwaka moto na hiyo humfanya mwanamke wa aina hiyo kuwa na hasira za mara kwa mara ambazo husababisha amani kutoweka ndani ya mioyo yao.

“Huu ni utafiti wa kitaalamu ambao nimeufanya katika mikoa mbalimbali ya Tanzania na nchi ya jirani na kubaini matokeo haya, “anasema Dkt. Mkombozi.



*TIBA

Kuhusu tiba Dkt. Mkombozi anasema magonjwa haya yanatibika kutokana na kuwa unapofanya utafiti wa jambo na kugundua tatizo ni lazima utafute suluhisho la jambo hilo.

Anasema kuwa wakati akifanya utafiti huo alikuwa akijaribu pia kutafuta ufumbuzi wa matatizo hayo na hivyo kugundua njia mbadala ya kukabiliana nayo.

“Huwezi kufanya utafiti na ukabaini jambo baya bila kutafuta mbadala wake na hivyo tumejaribu kutafuta suluhu hiyo na imepatikana,” anasema Dkt. Mkombozi.


Kwa Mawasiliano zaidi unaweza kumpata katika Namba zifuatazo:-

    +255 719 555 777      au    +255 782 357 978    au    +255 769 530 388